STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 6, 2018

Rostand anatunguliwa na kipa mwenzake

YANGA wanafungwa bao la nne kwa mkwaju wa penalti iliyopigwa na Zammamouche na kuifanya USM kutoka na ushindi mnono wa mabao 4-0. Pambano limeisha mara baada ya mkwaju huo.

Waarabu wanapata penalti

USM wanapata penalti baada ya Dante kucheza faulo ndani ya lango lake.

Zimeongezwa dakika mbili

ZIMEONGEZWA dakika mbili kabla ya pambano la Yanga na USM Alger kumalizika na matokeo bado ni 3-0.

Dante ameumia

BEKI na nahodha wa mchezo wa leo, Dante ameumia na anapatiwa matokeo. Bado dakika mbili mpira kumalizika. Yanga wapo nyuma mabao 3-0. Yohana Mkomola pia kaingia kuchukua nafasi ya Yusuf Mhilu aliyeshindwa kabisa kufurukuta.

Pato anaingia kumpokea Makapu

YANGA imefanya mabadiliko kwa kumtoa Juma Said 'Makapu' na kuingia Pato Ngonyani. USM Alger wamebanwa kwa sasa, lakini bado wanaongoza kwa mabao 3-0.

Darfalou alimwa kadi naye

Oussumana darfalou naye anapewa kadi ya njano kwa kumchezea Abdallah Shaibu Ninja anayekaba hadi kivuli. Dakika ya 70. Mabao bado 3-0.

Juma Mahadhi apewa kadi

JUMA Mahadhi anakuwa mchezaji wa kwanza kupewa kadi ya njano katika mchezo huu, Matokeo bado 3-0.

Rafael anatoka Abdul anaingia

Juma Abdul
YANGA imefanya mabadiliko ya kumtoa Rafael Daud na kumuingiza Juma Abdul ikiwa ni mbinu ya benchi la ufundi la Yanga kuimarisha ulinzi baada ya kuona wasipokuwa makini watapigwa nyingi.
Dakika ya 65' USM 3 Yanga 0

Yanga inapigwa la tatu


MAMBO yanazidi kuwa magumu kwa Yanga baada ya wenyeji kuandika bao la tatu, kutokana na uzembe wa mabeki na kipa Rostand na Abderrahmane Meziane anauweka kimiani mpira ikiwa ni dakika ya 54.
USM Alger 3 Yanga )

Hassan Kessy anaupiga mwingi

BEKI Hassan Kessy ndiye pekee anayeonekana kujitoa uwanjani akihakaka kila mahali.

Waarabu wameanza uhuni wao

MMOJA wa wachezaji wa USM Alger anafanya uhuni wa kupiga mpira na kumgandishia mguu beki Dante na kumfanya apatiwe matibabu. Hata hivyo Dante anaendelea. Matokeo bado 2-0.

Mopira umeanza

Dakika 45 za pili zimeanza, na Yanga wanafika langoni mwa USM Alger. Matokeo bado 2-0.

Timu zinarudi uwanjani

TIMU za Yanga na USM Alger zinarudi uwanjani kuanza kipindi cha pili.

Takwimu za nusu ya kwanza

USM Alger                        Yanga
2              Goals                 0

9              Shots                 3
3              Shots on Target   1
73%         Possession         27%
0              Yellow Card         0
0              Red Card             0
1              Offsides               2
7              Corners               1   

Ni mapumziko sasa

Pambano la Yanga na USM Alger limemaliza dakika 45 na wachezaji wanaenda mapumziko kupewa mawaidha kabla ya kurudi uwanjani kwa kipindi cha pili. USM wapo mbele kwa mabao 2-0.
Wenyeji wameposses mpira kwa asilimia 73 kwa 27 za Yanga.

Imeongezwa dakika moja ya nyongeza

Imeongezwa dakika moja kabla ya mapumziko, Yanga bado ipo nyuma kwa mabao 2-0

Yanga wanakosa bao

Shuti la Mwashiuya linaokolewa na kipa na kuinyima Yanga bao. Bao 2-0

Pengo la Tshishimbi, Chirwa, Ajibu laonekana


Bado dakika tano kabla ya mapumziko, lakini Yanga bado inahaha kurejesha mabao waliyotanguliwa na wenyeji wao, huku mapengo ya nyota watano waliobaki jijini Dar es Salaam yakionekana wazi.
Nyota hao waliokosekana kwenye mchezo huo unaoendelea mjini Algiers ni Papy Kabamba Tshishimbi, Obrey Chirwa, Kelvin Yondani, Ibrahim Ajibu na Thabani Kamusoko.

Mambo bado magumu

Pambano la Yanga na USM Alger bado linaendelea na Yanga wanapigwa bao la pili baada ya kona ya wenyeji kusindikizwa wavuni na Farouk Chafai dakika ya 33 kipa Rostand akifanya makosa yale yale na kufungwa bao rahisi. Mpira wa Chafai unamaliziwa kimiani na Pius Buswita.
USM Alger 2 Yanga 0

Yanga inapata kona ya kwanza

Yanga wanapata kona baada ya shambulizi lao kuokolewa na mabeki, wakati Geofrey Mwashiuya akijiandaa kufunga. Hata hivyo haijazaa matunda. Dk 26

Uwanja umeelemea kwa Yanga

DK 25 Yanga bado wanakimbizwa, licha ya kujitahidi kurudisha mashambulizi, lakini ni kama uwanja umeelemea upande mmoja.
Bao matokeo ni 1-0 wenyeji wapo mbele.

Yanga chupuchupu tena

Yanga chupuchupu wapigwe bao la pili, makosa ya Andrew Vincent 'Dante' na kipa Rostand ambaye amekuwa akitoka ovyo langoni mwake bila hesabu makini.
Dk 23

Yanga wanakoswa koswa

WAWAKILISHI wa Tanzania Yanga, bado wanashambuliwa na USM Alger, huku ikionekana upande wa kushoto unaolindwa na Gadiel Michael ukiwa uchochoro wa mashambulizi mengi ya wenyeji.
Dakika ya 21

Dakika ya 15 mambo bado

Matokeo bado ni 1-0 wenyeji wakiwa mbele, huku nyota wa Yanga wakionekana kuzidiwa na wenyeji.

Yanga yatanguliwa bao la mapema

DAKIKA ya Nne tu, Yanga wamesharuhusu bao la kuongoza la Waarabu wa USM Alger baada ya mabeki na kipa Youthe Rostand kushindwa kuokoa krosi pasi iliyoungwa na Oussama Darfalou
USM Alger 1 Yanga 0.